Mr Blue asema hahitaji meneja kwenye muziki wake



Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Mboga Sana’ amesema alikuwa hawezi kuishi kwenye tasnia ya muziki bila kuwa na meneja lakini kutokana na kuona mchango wao kwake haukuzaa matunda.
“Mimi nilikuwa siwezi kuendesha maisha yangu ya muziki bila kuwa na meneja na nilifanya kazi chini ya mameneja watatu lakini kwa sasa nimesema basi sihitaji meneja tena nahitaji ushauri wa wadau namna ya kuboresha kazi zangu,” Mr Blue alikiambia kipindi cha FNL cha EATV.
Rapa huyo pamoja na AliKiba wameshiriki kusapoti ngoma ya Abby Skills inayokwenda kwa jina la Averina , ambapo Abby amewataka mashabiki kumuunga mkono ili arejee vyema kwenye game kama zamani.