Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema wanaofanya vitendo vya uhalifu katika maeneo yao kuacha mara moja kutokana na operesheni inayotarajiwa kufanyika siku za hivi karibuni ikiwemo katika maeneo ya kigogo jijini Dar es salaam.
Hatua hiyo inakuja katika ziara ya Mkuu wa Mkoa Paul Makonda alipokuwa akihitimisha ziara ya siku kumi katika Wilaya ya Kinondoni ambapo jeshi hilo limewataka wazazi kukanya watoto wao kwa vitendo wanavyovifanya ikiwemo ni pamoja na ukabaji wa raia kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wakaazi wa eneo hilo ambapo wamedai kuwa watoto wa viongozi katika maeneo hayo wanaojishuhulisha na vitendo vya uhalifu pasipo kuchukuliwa hatua za kisheria.
Aidha Kamanda Sirro amesema kuna baadhi ya watu wanawatambua wahusika wanaofanya matukio ya uhalifu katika mitaa yao lakini hushindwa kutoa ushirikianao wa kutosha kwa jeshi hilo jambo ambalo huwakwamisha.