Tausi Mdegela: Watoto wakiniona wanatafuta vitenesi tucheze

Mwigizaji wa bongo muvi kwa upande wa komedi Tausi Mdegela amesema, mara nyingi akiwa sehem za matembezi, watoto wengi wanamkimbilia na wengine kutafuta vitenesi ili wacheze wakidhani supastaa huyo ni mtoto mwenzao.



Watoto wengine wanakuwa wanawasumbua wazazi wao(mama zao) wawanunulie nguo kama alizovaa Tausi. Tausi amesema anapenda sana watoto na muda si mrefu anategemea kufunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu japokuwa hakusema ni lini. Ameongezea pia mchumba ambae anatarajia kufunga nae ndoa ana kimo kirefu mwenye kuweza kuzima taa wanapokuwa chumbani. Muigizaji Tausi ameongea haya wakati anahojiwa na Dina Marios katika kipindi cha uhondo E fm radio.