JAY DEE: Ruksa kupiga Nyimbo za Jide, Bifu la Jay Dee na Clouds Limekwisha

Lady Jay Dee na Clouds Media Group hakuwa kwenye uhusiano kwa takribani zaidi ya miaka 4 na Nyimbo za Jay Dee kutokupigwa kwenye redio na Tv. Lady Jay Dee alipoulizwa kuhusu kauli ya Ruge kuwa tayari kupiga Nyimbo zake. Jay Dee akasema Uongozi wake ndio utakaotoa Majibu kuhusu kauli ya Ruge.

Jay Dee na Ruge


Sasa habari kubwa kwa sasa ni kauli ya Management ya Lady Jaydee ikiwa ni baada ya Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji Clouds Ruge Mutahaba kusema kwamba nyimbo za Jide zinaweza kuendelea kupigwa iwapo yeye mwenyewe ataruhusu maana alikataza na jina lake lisitajwe.

Uongozi wa Jay Dee umetoa taarifa na Kusema kuwa ni Ruksa kwa Clouds Media Group kuanza kupiga Nyimbo za Jay Dee muda wowote. Na kwamba wagange yajayo na kusahau yaliyopita.