Madereva hao walikamatwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo Geita, Arusha, Kilimanjaro, Kagera, Mara, Tabora, Lindi, Iringa, Shinyanga, Rukwa na Njombe baada ya operesheni iliyofanyika wiki tatu na ambayo inaendelea katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.
Mpinga amasema operesheni hiyo imefanyika katika barabara kuu zote, stendi za mabasi mikoa yote kwa kukagua ubora wa mabasi, mikanda, kuwapima madereva ulevi na uzidishaji wa abiria na nauli.