Taarifa iliyotolewa leo (Alhamisi) na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Jaji Kaijage ameteuliwa kuongoza NEC kwa miaka 5, kuanzia Desemba 16, 2016.
Jaji Kaijage anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Damiani Lubuva ambaye muda wake wa kuwa mwenyekiti wa tume hiyo ulimalizika Desemba 19, mwaka huu.