UTAFITI: NJAA KALI SUDAN KUSINI

Utafiri mpya uliofanywa na washirika wa masuala ya chakula na lishe unaonyesha kwamba watu takribani 260,000 mjini Juba Sudan Kusini ama wana chakula kidogo sana au hawana uhakila na mlo wao.



Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA inasema hali ya kutokuwa na uhakika wa chakula mjini Juba imeongezeka mara mbili tangu Julai mwaka jana.