Mtanzania Alphonce Feilix Simbu jana alifanikiwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mashindano makubwa ya riadha ya Mumbai Marathon.
Mkimbiaji huyo chipukizi alitumia saa 2:09:32 kukimbia mbio nzima. Felix pia alishiriki mashindano ya Olympic mwaka jana alishika nafasi ya 5 katika michuano ya Olympic.