Mambo 6 ya Kujifunza Katika Darasa la Fursa na Tigo Fiesta Mtwara ili uweze Kuongeza Thamani

Weka Malengo ya Muda mrefu na Mfupi
Kile unachoanza nacho kitazame kama kampuni fikiria baada ya miaka 10 mtakuwa wapi muhimu muwe na malengo sahihi. 

 "Ukiwa mjasiriamali lazima utazame mambo matatu. 
1. Lazima biashara ikue
2. Biashara iwe katika Ubunifu
3. Biashara  iwe na Faida"-
#RugeMutahaba akizungumza kwenye darasa  la #Fursa
#RugeMutahaba






Ili uweze kufanikiwa unatakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuacha uvivu
"Maisha yoyote yale ili ufanikiwe usijihurumie kufikiri unatakiwa kujituma achana na uvivu wa kufikiri" - Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Sebastian M.Walyuba.

Usisubiri kupata kikubwa, anza na kidogo ulichonacho
Nilikutana na Ruge Mutahaba Tabora ni kijana kama mimi ila amenipa motisha ya kujituma zaidi katika maisha.
Nilianza na ufugaji wa Kuku wawili wa kupewa sikuwa na Elimu ya Ufugaji bali nilijifunzia katika ufugaji wa kawaida tu.

Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Yahaya Nawanda, akizungumza kwenye darasa la Fursa Jinsi ya kuongeza thamani katika mifugo na Kilimo.

Usifanye Biashara kwa Mazoea
Biashara haina msiba lazima ujue biashara inatakiwa kuwepo kila siku ifanye biashara yako ya uhakika kama benki huu ndio upekee.

Charlz Nduku akizungumza na washiriki wa Semina ya #Fursa2016 #Mtwara kuhusiana na Brand.

Yajue Mazingira yako kuna Fursa
Tengeneza mfumo sahihi wa kukuza na kuimarisha biashara yako kwa kuyafahamu mazingira yako na changamoto zilizopo.

Watu wengi waneshindwa kutengeneza mfumo sahihi wa kukopesheka.
Mjomba @mrishompoto

Kuwa Na Maarifa ni muhimu katika Biashara na kuwa na maono
Ili ufanye biashara lazima uwe na pembe tatu salama watu wengi wanangamia kwa kukosa maarifa tu. Siku zote mafanikio hayana umri.

Hela ipo mwanzo hela ipo mwisho tunatafuta hela tukasome then tunatafuta kazi tupate hela hivyo hela sio msingi wa kufanikiwa. 

Kama kikundi lazima uwe na Mission itakayokupeleka kwenye Vision haya yote hayakamiliki bila kuwepo kwa team work.
@mrishompoto

hhhhhhhhhhhh