KIJANA ALIYEKOSA MKOPO AKILIA NA HABARI YAKE KUSAMBAA KUPITIA GAZEI LA MWANANCHI APATA MSAADA

Ni Wiki imepita toka kusambaa kwa picha ya kijana aliyekosa mkopo huku akiwa analia ikisambaa mtandaoni. Hatimaye kijana huyo amepata wasamalia wema ambao wamejitolea kumsomesha Elimu ya juu. Hii inakuja baada ya Mwnansheria Albertmsando kupost picha yake ya kutaka kuonana naye ili aweze kumsaidia.

Albert Msando ameandika haya kwenye kurasa yake ya Instagram
Mungu ni mwema. Nimempata kijana Edson Mwakyombe ambaye jana alilia kwa huzuni na uchungu kukosa mkopo ili aendele na Elimu ya Juu. Nimekutana nae Chuo Kikuu Mlimani. Ni baada ya kuweka post kuhusu Elimu ya Juu kijana huyu ambaye mama yake anaishi Mfinga Iringa na hana ndugu Dar Es Salaam leo amepata mama @isariaclothingboutique na kaka @furnituremart_ ambao wamejitolea kumlipia ada mwaka wa kwanza na wa pili. Nawashukuru sana kwa moyo wao wa kujitolea. Tuendelee kuwasaidia na wengine ambao wanalia na kuhuzunika bila msaada. Ni wengi lakini kila anaeguswa ajitoe na kumsaidia yule mwenye kuhitaji. #LetUsHelpEdoLearn #IsariaMlaki #AndrewKomba - by @albertomsando

Kijana mwenyewe huyo aliyevaa Begi akiwa na Wasamaria wema