Kipindi cha pili Stand United walisawazisha goli hilo kupitia mkwaju wa penati baada ya mchezaji wao kuchezewa vibaya ndani ya boksi la Simba. Matokeo hayo ya 1-1 yalidumu mpaka dakika 90 za mchezo na kuongezewa dakika 30 nyingine ambapo hakuna timu iliyoweza kuongeza goli
Baada ya kumalizika kwa dakika 30 za niongeza timu hizo zilikwenda kwenye hatua ya penati ambapo Simba waliibuka na ushindi wa jumla ya goli 8-7 kwa mikwaju ya penati
Matokeo hayo kwa Simba yanawasogeza kucheza fainali siku ya jumapili tarehe 11/12 mwaka huu na mshindi atakae patikana kwenye mchezo wa Azam dhidi ya ya Mtibwa Sugar unaochezwa leo usiku.