TANESCO: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuufahamisha Umma kuwa liko katika hatua mbali mbali za mabadiliko ya Uongozi wa ndani ya Shirika kwa lengo la kuongeza ufanisi zaidi.

Kwa msingi huo, mabadiliko yanayoendelea ndani ya Shirika yatawekwa wazi kwa wakati muafaka kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Shirika kwa kupitia vyombo vya habari. Hivyo tunaomba vyombo vya habari vitoe fursa kwa Mamlaka husika kuendelea kukamilisha zoezi hili muhimu kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla na taarifa rasmi itatolewa baada ya zoezi kukamilika. IMETOLEWA NA: OFISI YA UHUSIANO TANESCO - MAKAO MAKUU 05 Januari 2017.