ELIMU BIASHARA: Kwanini Mahari Sio Kigezo cha Upendo kwa wanandoa



Desturi ya kudai mahari kutoka  kwa MTU anaetaka  kuoa  ni utamaduni na mila za kale zinazoendelea miongoni mwa  watu na makabila mengi duniani. Kwa asili mahari ilikuwa ni  dhamana kwamba atakayeolewa atathaminiwa na kuhesabiwa kuwa  Mke halisi na hivyo kutendewa vizuri, kwa kadri mahari ilivyokuwa kubwa,ndivyo Mke alivyojiona wa  thamani zaidi. Lakini mambo yanatakiwa kubadilika, Msingi  wa  ndoa ni  Upendo .Upendo huo  ni  wa thamani kubwa sana na wa  kudumu kuliko mifugo, pesa au vitu vyovyote vitolewavyo kama mahari.

Hivyo watu wanao mjua Mungu wanaoana kwa Upendo wa  kweli hawana haja ya kuwa na dhamana nyingine ya usalama wa ndoa yao. Inashangaza na kusikitisha kuona baadhi ya wazazi hudai mahali kubwa ili  kujipatia mali kupitia watoto wao. Mahari kubwa sana hudaiwa kwa anaetaka Kuoa. Na ndo mana Vijana wa sikuhizi wengi wanachelea kuoa kwa sababu inawachukua takribani miaka mitatu kujipanga kimaisha, na takribani miaka mitatu mingine Kujipanga na mahari na harusi.

Sio Kwamba Mahari zisiwepo, Hapana, bali mahari isiwe kikwazo cha kuwaruhusu wawili waliopendana washindwe kuanza maisha ya Familia, ifike Pahali mahali iangalie na uwezo wa muoaji. Kijana kaenda Ukweni katajiwa Mahari Milioni tatu au Nne, bado Tanzanite ya Engagement, bado hajaambiwa alishe ukweni siku ya Mahari. Akirudi nyuma anakumbuka kuna gauni la kitchen party na send off ya bi harusi, Bado kuna suti yake, gauni la mkewe n nguo za wasimamizi wao. Hapo bado wageni wa mkoani na kuhudumia nyumbani. Akipiga hesabu anajikuta ana Bajeti ya zaidi ya Milioni Saba ndani ya miezi mitatu ya Mahari, Send Off na Ndoa.

Tag waoaji na waolewaji Watarajiwa.

Mwnadishi: Man Deo

Instagram: @elimu_biashara