GWAJIMA, WENZAKE KUJITETEA KORTINI LEO


Askofu mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,Josephat Gwajima na wenzake watatu  wataendelea kujitetea leo katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es salaam

Wakili wa serikali, Joseph Maungo alimweleza,Hakimu mkazi  mkuu, Goefrey Mwambapa kuwa kesi ilipangwa jana kwa ajili ya utetezi na wapo tayari

Gwajima pamoja na wenzie  wanatetewa na Wakili Peter Kibatala na Faraja Mangula, ambao wote walikuwepo mahakamani jana lakini hakimu mfawidhi, Cyprian Mkehe anayeisikiliza kesi hiyo hakuwepo

Katika kesi hiyo Askofu Gwajima anakabiliwa na shtaka la kushindwa kuhifadhi silaha na risasi anazomiliki kihalali katika usalama

Aidha Wenzie George Milulu, George Mzava (Msaidizi wake) na Yeriko Bihagaze  wanakabiliwa  na mshtaka ya kumiliki bastola aina ya Berretta na risasi 20 kinyume na sheria